📌 Dkt. Biteko Kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi Arusha
Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko leo Aprili 22, 2025 amewasili mkoani Arusha kwa ajili ya ziara ya kikazi ya siku tano ambapo anatarajiwa kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara.
Aprili 23 hadi 26, 2025 Dkt. Biteko atatembelea miradi ya Maji, Elimu, Hospitali na kuzungumza na wananchi kupitia mikutano ya hadhara katika Wilaya za Arusha, Arumeru, Longido na Monduli.
Aidha, ziara hiyo ya kikazi ya siku tano ya Dkt. Biteko ni sehemu ya Maadhimisho ya Miaka 61 ya Muungano Muungano.
MWISHO
No comments:
Post a Comment