KIKWETE AZINDUA ZOEZI LA KUPANDISHA MWENGE WA UHURU MLIMA KILIMANJARO KAMA ILIVYOELEKEZWA NA RAIS SAMIA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Wednesday 16 October 2024

KIKWETE AZINDUA ZOEZI LA KUPANDISHA MWENGE WA UHURU MLIMA KILIMANJARO KAMA ILIVYOELEKEZWA NA RAIS SAMIA







Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Tanzania inapeleka mwenge wa uhuru juu ya mlima Kilimanjaro ili kuitangazia dunia kuwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ni imara na pia itaendelea kulinda Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Aidha, Waziri Ridhiwani Kikwete amesema kuwa kwa mwaka huu 2024, Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameamuru mwenge wa uhuru upelekwe juu ya Mlima Kilimanjaro baada ya kuhitimisha mbio zake kwa siku 195.

Mhe. Ridhiwani amesema hayo Oktoba 15, 2024 katika hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro wakati wa hafla ya kupokea kikosi maalumu cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) ambacho kimepewa jukumu la kupeleka Mwenge wa Uhuru na Bendera ya Taifa la Tanzania kilele cha mlima Kilimanjaro.

Vile vile, Waziri Ridhiwani Kikwete amehamasisha vijana kuendelea kuenzi falsafa za mwenge wa uhuru ulioasisiwa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere mwaka 1961.

Awali akizungumza, Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana amesema kupandishwa mwenge wa uhuru mlima Kilimanjaro mwaka huu 2024 kunaleta hamasa ya uzalendo kwa wananchi hususan wakati huu ambao Tanzania inaadhimisha miaka 60 ya uhuru na mafanikio ya Taifa.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Babu amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuridhia mwenge wa uhuru kupandishwa kwa mara nyingine katika kilele cha mlima Kilimanjaro.

Kwa upande wake, Kiongozi wa hicho Maalum, Luteni Kanali Khalid amemhakikishia Mhe. Waziri Ridhiwani Kikwete kuwa kikosi hicho kitafikisha kinaulinda na kuutunza Mwenge wa Uhuru na Bendera ya Taifa la Tanzania hadi katika kilele cha mlima Kilimanjaro.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso