MKUU WA KITUO CHA ZIMA MOTO KAHAMA ATOA ELIMU YA MAJANGA YA MOTO KWA KINAMAMA HOSPITALINI KAGONGWA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Wednesday 4 September 2024

MKUU WA KITUO CHA ZIMA MOTO KAHAMA ATOA ELIMU YA MAJANGA YA MOTO KWA KINAMAMA HOSPITALINI KAGONGWA

 




NA PAUL KAYANDA, KAHAMA


Mkuu wa kituo ch Zimamoto na Uokoaji Wilaya ya Kahama, Mkaguzi Msaidizi Hafidhi Omari, ameendesha semina maalum katika Kituo cha Afya Kagongwa kwa ajili ya kutoa elimu kwa wanawake kuhusu vyanzo vya moto majumbani, Lengo  kuwasaidia wanawake kujikinga na majanga ya moto ambayo yamekuwa yakisababisha hasara kubwa na kuhatarisha maisha katika jamii.


Omari alieleza  vyanzo vya moto ni pamoja na  uendeshaji wa shughuli za jikoni bila tahadhari kama matumizi  ya gesi yasiyo salamavifaa vya umeme visipofanyiwa matengenezo mara kwa mara vinavyoweza kusababisha moto ambapo ameshauri  
kuwa na vifaa vya kuzima moto majumbani na kuelewa namna ya kutumia vifaa hivyo endapo kutatokea dharura.
 


Kina mama walioudhuria semina hiyo walipata fursa ya kuuliza maswali na kupata ufafanuzi wa kina juu ya hatua bora za kuchukua ili kujikinga na majanga ya moto. Aidha, walipongeza jitihada za Jeshi la Zimamoto na Uokoaji kwa kutoa elimu hiyo muhimu ambayo itawasaidia katika kulinda maisha yao na mali zao.


Omari aliahidi kuendelea kutoa elimu na kuhamasisha jamii kuhusu njia bora za kuzuia na kukabiliana na majanga ya moto ili kupunguza athari  katika Wilaya ya Kahama.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso