ALIYEJINYONGA AKIDAIWA KUMBAKA MJUKUU WAKE, AACHA UJUMBE MKE NA WATOTO WASIMZIKE - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 5 September 2024

ALIYEJINYONGA AKIDAIWA KUMBAKA MJUKUU WAKE, AACHA UJUMBE MKE NA WATOTO WASIMZIKE





Babu anayetuhumiwa kumbaka mjukuu wake wa miaka minane na kisha kujiua kwa kujinyonga baada ya mke wake kumfuma, aliacha ujumbe mkewe huyo, Philipina Olomi pamoja na watoto wake sita wasimuwekee udongo kwenye kaburi lake siku ya maziko yake.


Mzee huyo ambaye ni mkazi wa kijiji cha Kifuni, kata ya kibosho Magharibi, Wenseslaus Ulomi (50) anadaiwa kuchukua uamuzi huo wa kujiua baada ya kubaini mkewe amefahamu alimbaka mjukuu wake huyo, anayesoma darasa la kwanza katika moja ya shule iliyopo kijijini hapo akihofia aibu na kuchukuliwa hatua nyingine za kisheria.


Septemba 3, 2024, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa alithibitisha kutokea kwa tukio hilo akisema lilitokea Septemba 2, 2024 na kwamba mwanaume huyo alijiua kwa kujinyonga kwa kutumia shuka ambalo alilifunga juu ya kenchi ya chumba chake.


"Mnamo Septemba 2, mwaka huu huko kijiji cha Kifuni, kata ya Kibosho Magharibi Wenseslaus Olomi alibainika kujinyonga kwa kutumia shuka ambalo alilifunga juu ya kenchi ya chumba anachoishi na chanzo cha tukio hilo ni mgogoro wa kifamilia uliosababisha mwanaume huyo kuchukua maamuzi hayo," alisema Kamanda Maigwa.


Soma zaidi katika tovuti ya Mwananchi

(Imeandikwa na Janeth Joseph)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso