MICHANGO YA WATANZANIA YAMTOA GEREZANI ALIYECHOMA PICHA YA RAIS SAMIA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Tuesday 9 July 2024

MICHANGO YA WATANZANIA YAMTOA GEREZANI ALIYECHOMA PICHA YA RAIS SAMIA

Siku nne  tangu kijana Shadrack Chaula [24] aliyechoma picha ya Rais kuhukumiwa kulipa faini ya Sh millioni 5 au kifungo cha miaka miwili jela , hatimaye michango ya wananchi imefanikiwa kumtoa  katika Gereza  la Ruanda Mkoa lililoko Mkoani Mbeya.



Shadrack aliyekamatwa  kwa  madai  ya  kuchoma picha ya Rais Samia Suluhu Hassan na kushitakiwa kwa kosa  la kutoa taarifa  za uongo, alikwenda Gerezaqni baada ya kushindwa kulipa faini  hiyo.


Akizungumza baada ya kutoka  katika Gerezani la Ruanda akiwa na ameambatana na Wakili wake Michael Mwangasa, Kijana huyo ambaye ni Msanii wa Sanaa ya uchoraji amewashukru Watanzania kwa kuchanga fedha na kumtoa Gerezani.


“Nawashukru Watanzania kwa upendo wa kunichangia Fedha na mawakili  mlionihangaikia kuja kunitoa gerezani wote nawaombea kwa Mungu awabariki  sana” amesema Shadrack huku akiwa na uso wa furaha.


Kwa upande wake, Wakili aliyekuwa  akishughulikia suala hilo, Michael Mwangasa amesema  wana nia ya kukata Rufaa katika Mahakama kuu kanda ya Mbeya


“Hatujaridhika na hukumu iliyotolewa kwa sasa tunaweka mambo sawa hasa taratibu zote za kisheria kabla ya kwenda kukata rufaa katika mahakama kuu kanda ya Mbeya” amesema Mwangasa


Kijana huyo alipofikishwa mahakamani, alisomewa shitaka la kutoa na kusambaza taarifa za uongo kupitia mtandao wa kijamii TikTok, kosa ambalo ni kinyume cha sheria ya  makosa ya mtandao kifungo cha 16

 

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mkuu Mahakama ya wilaya Rungwe Mkoa wa Mbeya, Shamla Shehagilo, baada ya mshitakiwa huyo, mkazi wa kijij cha Ntokela, Wilayani humo  kukiri kosa hilo.


Baada ya kukiri ya kosa hilo, Hakimu Shehagilo alimtia hatiani kwa kosa hilo na kumuhukumu kulipa faini Sh  millioni 5 au kwenda jela miaka miwili.


Awali, Mwendesha Mashtaka wa Serikali, Rosemary Mgenije, aliyekuwa akisaidiana na wakili Veronica Mtafya, alidai juni,  22, 2024 eneo  Ntokela lililopo kata ya ndato wilaya ya  Rungwe Mkoani Mbeya, mshitakiwa alitenda kosa hilo kupitia  akaunti yake ya mtandao kijamii@jet.fightershop  akiwa ameshika picha inayomwonesha Rais Samia, Akisema


“Kwa kuwa umeshindwa kutetea haki Taifa lako lisiathirike na ushoga, hii video inakuhusu wewe na si mtu mwingine wakati ukijua taarifa hizo ni uongo na upotoshaji kwa jamii” amedai Wakili Veronica

 

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso