KAMWE AMEJIUZULU NAFASI YA UMENEJA HABARI YANGA SC - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Monday 29 July 2024

KAMWE AMEJIUZULU NAFASI YA UMENEJA HABARI YANGA SC






Ally Shaban Kamwe baada ya kuhudumu kwa misimu miwili kama Meneja wa idara ya Habari na Mawasiliano Yanga SC ,leo ameandika barua ya kujiuzulu nafasi hiyo baada ya kuitumikia kwa mafanikio.

Kamwe alianza kazi Yanga September 25,2022 , leo July 29 amejiuzulu taarifa rasmi itatolewa muda wowote kuanzia sasa

Shaffi Dauda

=====



Ally Kamwe amepost haya kwenye ukurasa wake wa Insta akiwaaga mashabiki wa Yanga;

A Good dancer must know when to Leave a Stage.

𝑀𝑡𝑢𝑚𝑏𝑢𝑖𝑧𝑎𝑗𝑖 𝑚𝑧𝑢𝑟𝑖 𝑎𝑛𝑎𝑡𝑎𝑘𝑖𝑤𝑎 𝑘𝑢𝑗𝑢𝑎 𝑛𝑖 𝑤𝑎𝑘𝑎𝑡𝑖 𝑔𝑎𝑛𝑖 𝑤𝑎 𝑘𝑢𝑜𝑛𝑑𝑜𝑘a 𝐽𝑢𝑘𝑤𝑎𝑎𝑛𝑖..

Maneno ya hekima kutoka katika kinywa cha Patrick Loch Otieno Lumumba;

Na ni Hekima hii, inanituma mbele yenu Wananchi, Mashabiki na Wanachama wa Klabu yetu pendwa, kuwaambia kuwa, Ni wakati sasa wa kijana wenu kuondoka Jukwaani.

Nimesimama Miaka miwili juu ya hili Jukwaa, Tumeimba, Tumecheza, Tumefurahi na Alhamdulillah Tumeshinda pamoja kila pambano Lililokuja mbele yetu.

Muda wangu umemalizika na Asanteni sana.

Tutaonana tena Wakati mwingine nikiwa na kitu kizuri cha kuwaonyesha Juu ya Jukwaa.

DaimaMbeleNyumaMwiko.

Mwenyekiti wa Wasemaji

Ally Kamwe.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso