MAJALIWA: WATANZANIA TUENDELEE KUDUMISHA AMANI, UPENDO NA MSHIKAMANO - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Monday 17 June 2024

MAJALIWA: WATANZANIA TUENDELEE KUDUMISHA AMANI, UPENDO NA MSHIKAMANO





WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Watanzania kuendelea kudumisha amani, upendo, umoja, mshikamano, kuhurumiana sambamba na kujiepusha na vitendo vinavyoashiria vurugu, uonevu na uvunjifu wa amani.


Pia amewasihi waimarishe malezi kuanzia ngazi ya familia ili kuepuka athari za mmomonyoko wa maadili nchini na kuhakikisha mienendo ya vijana na wanajamii wote inazingatia mila, desturi na tamaduni zetu.


Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatatu, Juni 17, 2024) wakati wa hafla ya Baraza la Idd El-Adh’haa Kitaifa lililofanyika katika Msikiti wa Mfalme Mohamed VI Bakwata Makao Makuu, Kinondoni jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso