
Rai hiyo imetolewa na mwanafunzi kutoka Chuo cha Afya na Sayansi Shirikishi (Muhimbili), Yuda Sale ambaye pia amepongeza uongezwaji wa wafanyakazi katika vyuo akisema unachangia kuongeza ufaulu wa wanafunzi kwa kiwango kikubwa.
Kwa upande wake Alice Robert, mwanafunzi kutoka Taasisi ya Uasibu Tanzania (TIA) amepongeza utekelezaji wa bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2023/24 akisema wana matarajio makubwa kuwa kupitia bajeti ya mwaka wa fedha 2024/25 mageuzi makubwa katika sekta ya elimu yataenda kufanyika na kwamba wanafunzi watasoma katika mazingira bora zaidi.
No comments:
Post a Comment