TUNA MKAKATI MAALUM NA VISIWA VYA COMORO- PROF JANABI - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Tuesday 21 May 2024

TUNA MKAKATI MAALUM NA VISIWA VYA COMORO- PROF JANABI

Mkurugenzi  Mtendaji wa Hospitali ya Taifa ya  Muhimbili, Prof Mohamed Janabi amesema kuwa wana mkakati maalum wa kutoa huduma za kisasa za matibabu   kwa wagonjwa wanaofika hospitalini hapo kutoka visiwa vya Comoro kutokana na ongezeko la idadi yao katika siku za hivi  karibuni.


Prof Janabi amesema hayo alipokuwa akizungumza na Balozi Mteule wa Tanzania nchini Comoro, Ndg
  Saidi  Yakubu aliyefika kumuaga.



Prof   Janabi  ambaye pia ndio Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Utalii wa Matibabu ameeleza kuwa kwa hivi sasa wana mratibu maalum wa wagonjwa toka nje ya nchi na pia mkalimani wa lugha ya kifaransa ili kurahisisha mapokezi ya wagonjwa toka Comoro na wako tayari kuwa na kliniki za ufuatiliaji  kwenye visiwa hivyo.


“Kwa idadi yao na inavyoongezeka,tunakusudia tuwe na wodi maalum ya wagonjwa  wanaotoka Comoro katika siku za hivi  karibuni”  amesema  Prof Janabi.



Kwa upande
 wake, Balozi  Yakubu   ameahidi  kwenda  kufanyia kazi na kuwa na uratibu mzuri wa  wananchi wa  visiwa  vya Comoro kuja nchini kwa matibabu.

 

 

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso