MICHAEL COHEN AKIRI KUMWIBIA DONALD TRUMP DOLA 60,000 - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Wednesday 22 May 2024

MICHAEL COHEN AKIRI KUMWIBIA DONALD TRUMP DOLA 60,000

Aliyekuwa mshirika wa kisiasa wa Donald Trump,  Ndg Michael Cohen,  amekiri siku ya Jumatatu kuiba dola 60,000 kutoka kwenye utajiri mkubwa wa biashara za nyumba za aliyekuwa  Rais wa zamani wa Marekani  Donald Trump akidhani  kuwa   amemlaghai kuhusu kiwango cha bonasi yake ya mwisho ya mwaka 2016.

Michael Cohen, aliyekuwa mshirika wa kisiasa wa Donald Trump

 

Kukiri kwa Cohen kulikuja wakati akitoa ushahidi kwa saa kadhaa katika kesi ya jinai ya Trump huko New York,  Wakili wa utetezi wa Trump, Todd Blanche alimuuliza  maswali  Cohen ya kumlenga. Baadaye, mwendesha mashtaka Susan Hoffinger ametaka kurekebisha sura ya Cohen mbele ya jopo la mahakama la watu 12 kwa kumuuliza maswali yaliyolenga kufafanua majibu ya Cohen chini ya uchunguzi wa wakili Blanche ambao ulichukua siku tatu.


Blanche ameshambulia uaminifu wa Cohen, ambaye kwa miaka mingi amefanya kazi kushughulikia kila mahitaji ya Trump kabla ya kumgeuka mwaka 2018. Cohen, shahidi muhimu zaidi wa mwendesha mashtaka, wiki iliyopita alikubali kwamba kwa miaka mingi amekuwa akidanganya kwa niaba ya Trump na. hiyo imejitokeza tena katika ushuhuda wake wa Jumatatu.


Wizi wa pesa hizo kutoka kwenye Shirika la Trump, Cohen amekiri, ulichangia sehemu kuu ya kesi dhidi ya Trump, ambaye amekanusha mashtaka 34 yanayomkabili. Trump ndiye mgombea mtarajiwa wa urais wa chama cha Republican kwa mwaka 2024 dhidi ya Rais Joe Biden, Mdemocrat ambaye alipata ushindi dhidi ya Trump mwaka 2020.

 

 

 

 


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso