BASI LA KAMPUNI YA TAKBIR LAPATA AJALI LAJERUHI WATU 18 ENEO LA MANGA MKOANI SINGIDA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 23 May 2024

BASI LA KAMPUNI YA TAKBIR LAPATA AJALI LAJERUHI WATU 18 ENEO LA MANGA MKOANI SINGIDA

Basi la kampuni ya Takbir lililokuwa likitokea Dar es Salaam kuelekea Katoro mkoani Geita limepata ajali leo Mei 23, 2024 saa moja asubuhi katika eneo la Manga mkoani Singida na kujeruhi watu 18.



Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida, SACP. Amon Kakwale amesema majeruhi wa ajali hiyo wamepelekwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Singida kwa ajili ya matibabu.

Baadhi ya mashuhuda wamedai kuwa basi hilo limepata ajali baada ya kuyumba mara kadhaa na kugonga kingo za barabara na kisha kupinduka wakati likijaribu kulikwepa gari dogo lililokuwa limeegeshwa kando ya barabara.




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso