WANAWAKE WENYE ULEMALU WALIA NA CHANGAMOTO YA MASOKO YA BIDHAA ZAO, WAIANGUKIA UWT - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Friday 8 March 2024

WANAWAKE WENYE ULEMALU WALIA NA CHANGAMOTO YA MASOKO YA BIDHAA ZAO, WAIANGUKIA UWT


Wanawake wenye ulemavu wameiomba serikali kuwasaidia kutatua changamoto ya masoko ya bidhaa zao ili kuweza kujikwamua kiuchumi kutokana na kukosa masoko huku wakiwa wametumia nguvu na rasilimali kubwa kwenye utengenezaji wa bidhaa.


Wito huo umetolewa na wanawake wenye ulemavu wa kituo cha Udiakonia kilichopo Tandala wilaya ya Makete mkoani Njombe mbele ya mwenyekiti wa UWT mkoa wa Njombe Skolastika Kevela wakati wakiuza bidhaa zao kwenye sherehe kuelekea siku ya wanawake Duniani.


Hekima Mgeni ni kiongozi wa kikundi hicho ambaye pia anakabiliwa na changamoto ya ulemavu wa miguu anasema wao wanajishughulisha na kazi nyingi ikiwemo ushonaji wa vikapu,nguo,asali wanayoivuna kwenye mizinga yao takribani kumi waliyonayo lakini wanakabiliwa na changamoto ya masoko ya bidhaa zao.

“Tunatengeneza vikapu lakini pia mizinga tunayopalepale Udiakonia na tunapata asali mbichi,sisi kwenye kundi letu tuna viziwi ambao ndio wanaohusika kuweka mizinga na kupaka nta ila kwenye masoko yetu asali sio tatizo sana kwasababu watu wanajua umuhimu wake lakini vikapu soko bado”amesema Hekima


Naye mwenyekiti wa UWT mkoa wa Njombe amesema walemavu wamekuwa na mchango mkubwa kwenye maendeleo kwa kutengeneza bidhaa mbalimbali na kufanya shughuli kama watu wengine hivyo kuna umuhimu mkubwa kuuungwa mkono huku akiahidi kufikisha kwenye serikali changamoto za wanawake hao ili ziweze kufanyiwa kazi.


“Kina mama wenzetu hawa wanafanya kazi kubwa lazima tuwaunge mkono,niombe jamii iione changamoto hii na wadau mbalimbali waendelee kuwaona watu hawa na sisi kwa nafasi zetu lazima tuwasaidie”amesema Scolastika Kevela


Aidha katika kuadhimisha siku hiyo ya wanawake,Mwenyekiti kwa kushirikiana na wanawake wilayani Makete wamefanikiwa kutembelea na kuwaona wafungwa na Mahabusu walioko kwenye gereza la Ndulamo na kukabidhi mahitaji mbalimbali pamoja na kutoa taulo za kike kwa wanafunzi wa Sekondari ya Ilumaki




No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso