RAIS WA AWAMU YA PILI WA TANZANIA ALI HASSAN MWINYI KUZIKWA MACHI 2 VISIWANI UNGUJA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Friday 1 March 2024

RAIS WA AWAMU YA PILI WA TANZANIA ALI HASSAN MWINYI KUZIKWA MACHI 2 VISIWANI UNGUJA

Mwili  wa  aliyekuwa  Rais wa  Awamu ya Pili wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi, unatarajiwa kuzikwa tarehe  2  Machi 2024, mjini Unguja.

 



Ratiba ya mazishi ya marehemu Mwinyi imetangazwa  29 Februari 2024  na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, wakati akitangaza kifo chake.

 

“Kwa niaba ya Serikali ninatoa pole kwa familia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote kwa msiba huu mkubwa kwa Taifa letu. Nchi yetu itakuwa katika kipindi cha siku saba za maombolezo, ambapo bendera zitapepea nusu mlingoti kuanzia  Machi 1, 2024,  Hayati  Mzee Ali Hassan Mwinyi atazikwa tarehe 2 Machi 2024 huko Unguja,  kisiwani  Zanzibar ,” Amesema  Rais Samia

 

Inna Lillahi wa inna ilayhi raaji’un.”

 

Rais Mwinyi, amefariki dunia   Ijumaa    Februari  29, 2024 majira ya saa 11:30 jioni, katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Emilio Mzena, Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu ya ugonjwa wa Saratani ya Mapafu.

 

Ali Hassan Mwinyi  alikuwa Rais  wa awamu  ya pili wa Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania   kuanzia mwaka  1985  hadi  1995.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso