SERIKALI YA KUWAIT IMEKUA MSAADA KATIKA SEKTA YA AFYA NCHINI TANZANIA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 22 February 2024

SERIKALI YA KUWAIT IMEKUA MSAADA KATIKA SEKTA YA AFYA NCHINI TANZANIA

Serikali ya Kuwait imekuwa msaada kwa Serikali ya Tanzania katika Sekta ya Afya ambapo imeweza kusaidia mipango kadhaa ikiwa ni pamoja na kutoa msaada wa mashine za ganzi kwa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).


                          Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu




Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu  amesema hayo usiku wa jana Februari 21, 2024 Jijini Dar Es Salaam kwenye Maadhimisho ya Miaka 63 ya Uhuru na miaka 33 ya Siku ya Ukombozi wa Kuwait ambapo kwa Tanzania Maadhimisho hayo yameongozwa na Balozi wa Kuwait nchini Mhe. Mubarak Mohammad Alsehaijan.


“Kwa nafasi yangu kama Waziri wa Afya, kwa namna ya pekee kabisa  napenda kuishukuru Serikali ya Kuwait kwa msaada wake katika Sekta ya Afya  pamoja na kutoa msaada wa mashine za ganzi  wameweza kusaidia vifaa vya upasuaji kwa watoto wanaosumbuliwa na vichwa vikubwa (Hydrocephalus) kwenda Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI).” Amesema Waziri Ummy

 

 

    Mhe, Ummy  Mwalimu   na Balozi wa Kuwait   Mhe.                    Mubarak Mohammad Alsehaijan.



Waziri  Ummy  amesema  Kuwait imesaidia pia kwa kutoa Vifaa Tiba katika Hospitali ya Mnazi Mmoja Zanzibar, Mashine za Watoto Wachanga zisizo na hewa kwa Hospitali ya Benjamin Mkapa mjini Dodoma pamoja na ujenzi wa Hospitali ya Handeni Mkoani  Tanga  inayofadhiliwa na Taasisi ya Abdullah  Al Nouri ya Kuwait.


Aidha,  kwa mwaka  2023  Kuwait kupitia   Kuwait Children Heart Association ilileta madaktari bingwa walioshirikiana na watalaam wa Hospitali ya Benjamin Mkapa Dodoma na kufanya upasuaji wa moyo bure kwa watoto  100 wa kipato cha chini  Nchini.


“Hatua hizi zinaashiria kwamba uhusiano wa kindugu na urafiki uliopo kati ya nchi zetu mbili (Tanzania na Kuwait)  nina imani kuwa uhusiano huu utaendelea kuwa wa karibu na chini ya uongozi wa busara  mahiri na mwanga wa viongozi wetu wawili, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan na Sheikh Mishal al-Ahmad al. -Sabah, Amir wa Kuwait.” Amesema Waziri Ummy

 




Chanzo : Fullshangwe

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso