MAKAZI YA MWALIMU NYERERE KUWA KITUO CHA UTALII - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Wednesday 28 February 2024

MAKAZI YA MWALIMU NYERERE KUWA KITUO CHA UTALII

Serikali   imedhamiria  kuyafanya  makazi ya hayati Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage  Nyerere  yaliyoko kijiji cha Mwitongo, wilayani Butiama mkoani Mara kuwa kituo  cha utalii.

 


Hayo yamesemwa   Februari 27, 2024  na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa  wakati akizungumza na wakazi wa Kitongoji cha Muhumba, wilayani Butiama, akiwa njiani kuelekea Mugumu, Serengeti  ambako anaendelea na ziara yake ya kikazi mkoani Mara.


Waziri  Mkuu  Majaliwa  amemwagiza Mkuu wa Wilaya hiyo, Moses Kaegele atembelee  eneo, akagua na kuangalia mapungufu yaliyopo ili Serikali iweze kuyafanyia kazi. Pia ameiagiza wizara ya ujenzi ishughulikie  barabara ya kutoka Serengeti hadi Butiama ili ikamilike na kuwawezesha watalii wanaotaka kufika kwenye makumbusho hayo kwa njia ya barabara.


Waziri Mkuu alipitia Mwitongo na kuwasalimia wanafamilia wa Baba wa Taifa na kuweka shada la maua kwenye kaburi lake.

 

Mapema, alipowasili wilayani humo, Waziri Mkuu aliweka jiwe la msingi la ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Butiama ambayo utekelezaji wake umefikia asilimia 60.


Akizungumza mara baada ya kuweka jiwe hilo, Waziri Mkuu alimtaka mkandarasi wa mradi huo ambaye ni Wakala wa Majengo (TBA) ahakikishe anaukamilisha mradi huo kwa wakati. Hadi sasa, mkandarasi ameshalipwa sh. milioni 843.4 ikiwa ni malipo ya awali na hati  za  malipo ya pili na tatu.

 

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amesema Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea na kazi ya kupeleka umeme kwenye vijiji ambapo kazi kubwa imefanyika na sasa nguvu kubwa inaelekezwa kwenye kufikisha umeme kwenye vitongoji.

 

Akizungumza na wakazi wa Issenyi, wilayani Serengeti, akiwa njiani kuelekea Mugumu, Mheshimiwa Majaliwa alitoa rai kwa Watanzania waachane na matumizi ya kuni na mkaa na badala yake waanze kutumia gesi.

 

Chanzo : FullShangwe

  

 

 

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso