EPUKENI MATUMIZI YASIYO SAHIHI YA P2 - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Monday 19 February 2024

EPUKENI MATUMIZI YASIYO SAHIHI YA P2

 

Naibu Waziri wa Afya Dkt,  Godwin Mollel  amewataka wananchi kuepuka matumizi yasiyo sahihi ya vidonge vya kuzuia mimba maarufu kama P2  ili  kuepuka  madhara yanayoweza kujitokeza pale dawa hizo zinapotumika bila utaratibu ikiwemo mvurugiko wa hedhi. 




                                                                           

Dkt. Mollel amesema hayo leo Jijini Dodoma kwa niaba ya Waziri wa Afya  Mhe,  Ummy Mwalimu wakati akijibu swali Namba  163 ambapo  swali hilo limeulizwa na Mbunge wa Viti Maalum  Dkt, Thea Medard Ntara aliyeuliza Je, kuna mpango gani wa kuruhusu Sayana Press kama njia ya Uzazi wa Mpango  badala  ya kutumia P2 bila utaratibu.


P2 ni njia ya dharura ya vidonge vya uzazi wa mpango ambayo hutumika kuzuia mimba kwa mwanamke aliyefanya tendo  la kujamiiana bila kinga kwa mfano aliyebakwa,  au aliyetumia  kondomu ikapasuka na anadhani anaweza kupata mimba asiyoitarajia  wakati Sayana Press ni njia ya kuzuia kupata ujauzito kwa muda mrefu, aliseme Dkt Mollel


Hata hivyo Dkt. Mollel ameongeza kuwa Sayana Press imesajiliwa na  TMDA  na inapatikana kwenye vituo binafsi vya kutolea huduma za afya kwa wateja  wanaohitaji.


Chanzo : FullShangwe

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso