WAOMBA HUDUMA ZA KIBENKI KUTOKANA NA KUKITHIRI UCHIMBAJI MADINI. - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 24 June 2021

WAOMBA HUDUMA ZA KIBENKI KUTOKANA NA KUKITHIRI UCHIMBAJI MADINI.

 


IMEFAHAMIKA kwamba uongozi wa Kata ya Segese,katika Halmasahuri ya Msalala,wilaya ya Kahama,imefikia hatua ya kuomba huduma za Kibenki, kutokana na Kata hiyo kushamiri kwa shughuli za kibiashara zinazochagizwa na wingi wa wachimbaji wadogo wadogo madini ya dhahabu katika maeneo hayo.

 

Kata ya Segese ipo umbali wa kilometa 40 kutoka Kahama Mjini,kwenye huduma za kibenki,huku Kata hiyo ikiwa na mzunguko mkubwa wa kifedha,hivyo kuomba ngazi husika kuangalia uwezekano wa kufungua tawi dogo la Benki kurahisisha huduma za fedha mahali hapo.

 

Hayo yalibainishwa juzi na Mtendaji wa Kata ya Segese, John Mahona, wakati akiongea na Waandishi habari,juu ya usalama wa fedha ambazo wanakuwa nazo wachimbaji hao katika eneo hilo huku wengine wakitumia mabegi na mifuko badala ya kuweka katika taasisi za kifedha.

 


Mahona alidai eneo hilo lina mahitaji makubwa ya huduma za kifedha kwa ajili ya usalama wa Wachimbaji madini ya dhahabu, wanaopata tabu   kupata huduma za kifedha za kibenki na kulazamika kutembea umbali huo jambo ambalo linahatarisha maisha yao.

 

Mahona alisema kuwa katika kaya yake mbali na wachimbaji hao kumiliki fedha nyingi pasipo ulinzi wake pia kuna maduka mengi ya fedha fedha ambayo kimsingi wamiliki wake wamekuwa wakiaa na fedha nyingi bila ya kuhofoa usalama wao.

 

“….tuna mzunguko mkubwa wa fedha kutokana na madini yaliyopo,ni muhimu kukawa na tawi lolote la kibenki kwa usalama wa watu wa eneo hili,”alisema Mahona.

 

Hata hivyo Mtendaji huyo, alisema kumekuwa na ongezeko kubwa la  watu kutoka 20,000 hadi   kufikia   35,000 kutokana na machimbo hayo ya Ntambalale namba moja hadi tano ambayo watu wengi wanachimba madini ya dhahabu katika maeneo hayo.

 

Aidha alisema kuwa machimbo hayo yamesaidia pia kukuza uchumi kwa watu na mtu mmoja mmoja katika eneo hilo huku akiongeza kuwa hali hiyoimetokana na baadhi ya wachimbaji wadogo kupewa Leseni za uchimbaji katika maeneo hayo.

 

Alisema kuwa wachimbaji hao wameweza kusaidia katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo katika Kata ya Segese kama vile kujenga kwa gharama zao Zahanati katika kijiji cha Wisolele  na kuongeza kuwa pia wamejenga kituo cha Polsi katika Mji wa Segese.

 

Aliendelea kusema kuwa pia wachimbaji hao wameshiriki katika ujenzi wa vyoo vya matundu sita katika Shule ya Sekondari ya Mwalimu Nyerere,kutoa vifaa mbalimbali  ikiwemo kompyuta katika Shule ya Sekondari ya Segese na kusaidia ukamilikaji wake wa jengo la utawala.

 

 

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso