MAREKANI YARIDHISHWA NA MAGEUZI YA KIUTENDAJI YA SERIKALI YA RAIS SAMIA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Friday 18 October 2024

MAREKANI YARIDHISHWA NA MAGEUZI YA KIUTENDAJI YA SERIKALI YA RAIS SAMIA




Yaahidi kuendelea kutoa fedha kuisaidia Tanzania kutatua vikwazo vya ukuaji uchumi




Shirika la Changamoto za Milenia (Millennium Challenge Corporation-MCC) la Serikali ya Marekani limeeleza kuridhishwa kwake na mageuzi ya mifumo ya kiutendaji, yaliyofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita katika maeneo mbalimbali ikiwemo uimarishwaji wa demokrasia, utawala bora na haki za binadamu.




Hayo yamebainishwa wakati wa mkutano uliofanyika kati ya ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na ujumbe wa Shirika la Changamoto za Milenia uliofanyika terehe 17 Oktoba 2024 jijini Dodoma.




Akizungumza kwenye mkutano huo Bw. Dan Barnes, Mkurugenzi wa Sera na Tathmini wa shirika hilo ambaye pia ameongoza ujumbe wa Marekani kwenye mkutano huo, ameeleza kuwa katika kipindi cha miaka mitatu ya Serikali ya Awamu ya Sita, wameridhishwa na hatua mbalimbali zilizochukuliwa na Tanzania ambazo zimechangia kuongeza kasi ya maendeleo ya kiuchumi nchini.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso